Powered by RND
PodcastsGovernmentTANAPA PODCAST

TANAPA PODCAST

Tanzania National Parks (TANAPA)
TANAPA PODCAST
Latest episode

Available Episodes

5 of 18
  • TANAPA PODCAST EPISODE 16: MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
    Episodi hii inaangazia njia za asili zilizotumika katika utunzaji wa maliasili kwa kufuata taratibu za kitamaduni, mila, desturi na makatazo mbalimbali yaliyosaidia kusimika mizizi imara na kuwa chimbuko la uhifadhi wa kisasa. Hekima za mababu zetu kama vile kuheshimu misitu, kutotumia rasilimali kupita kiasi, na kutambua uhusiano wa binadamu na mazingira vimekuwa dira muhimu inayoongoza mbinu za kisayansi za leo kwenye uhifadhi endelevu. Sikiliza simulizi hii ya kuvutia katika Epsodi ya 16.Mwongoza kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena.Mgeni I: Mzee Rashid Shabani Kitopeni.Mgeni II: Mzee Ramadhani NyundoUsikose kila Jumatatu kupitia Platform za TANAPA Podcast.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.
    --------  
    35:37
  • UHIFADHI NI JUKUMU LA KILA MMOJA
    Episodi hii inakuletea uchambuzi wa kina kuhusu Uhifadhi kwa kuzingatia kuwa Uhifadhi wa wanyamapori ni zoezi la kujitolea kulinda na kuhifadhi maliasili kwa maslahi ya Taifa kwa kizazi hiki ma kijacho.Sikiliza Episodi ya 15 upate elimu kutoka kwa Mzee Ibrahimu Kasontola kutoka katika kijiji cha Lukoma wilayani Uvinza - Kigoma aliyejitolea kwa hali na mali kuhifadhi msitu katika eneo la makazi yake na kupelekea eneo hilo kuwa makazi ya kudumu ya Sokwemtu sanjari na kupanda migomba ambayo hutumika kama chakula pendwa cha wanyamapori hao ambao mara nyingi utawakuta katika makazi ya mzee huyo.Mwongoza Kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena.Wageni 1.⁠ ⁠Ibrahim Kasontola (Mzee anayewahifadhi Sokwemtu hao).2.⁠ ⁠Mwatano Omary (Mke wa Mzee Ibrahim Kasontola).3.⁠ ⁠⁠Afisa Uhifadhi Mwandamizi - Lameck Matungwa Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Milima MahaleUsikose kila Jumatatu kupitia Platform za TANAPA Podcast.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.
    --------  
    1:02:33
  • TANAPA PODCAST EPISODE 14: MILA, DESTURI NA TAMADUNI KATIKA UHIFADHI WA MALIASILI.
    Episodi hii inaangazia mila, desturi na tamaduni katika uhifadhi wa maliasili, hususan namna jamii ya Wangoni kutoka mkoani Ruvuma ilivyotumia majina na utamaduni wao kulinda Wanyamapori na Misitu  tangu enzi za mababu zetu.Hadithi hii ya kuvutia inaonesha jinsi urithi wa jadi ulivyokuwa chachu ya kulinda rasilimali za Taifa ambazo leo hii zinachangia kwa kiasi kikubwa katika sekta ya uhifadhi na utalii.Sikiliza simulizi hii adhimu kutoka kwa Chifu Songea Mbano wa Kwanza, kupitia TANAPA Podcast – Episode ya 14. Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine MbenaMgeni: Samweli Vitus Mbano (Chifu Songea Mbano I)Usikose kila Jumatatu na Alhamisi kupitia majukwaa mbalimbali ya TANAPA Podcast
    --------  
    55:20
  • TANAPA PODCAST EPISODE 13 - Mila na Tamaduni zilizohusisha mizimu katika kuhifadhi Maliasili
    Episodi hii inakuletea mazungumzo ya kina kuhusu mila, tamaduni na makatazo ya Kabila la Wagongwe lililopo mkoani Katavi na jinsi taratibu hizo zilivyochangia kulinda maliasili na vyanzo vya maji. Mathalani; ilikuwa hairuhusiwi kukata miti iliyokuwa katika vyanzo vya maji kutokaana na imani ya kuwepo kwa nyoka mkubwa wala kuua mnyamapori hadi upewe kibali na pepo au jini Katabi anayepatikana katika Hifadhi ya Taifa Katavi. Sikiliza simulizi hii ya kuvutia katika epsodi ya 13.Eneo: Hifadhi ya Taifa KataviMwongoza kipindi: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena Wageni:1.⁠ ⁠Moses Edward Tende ( Mtemi Sigulu) Chifu wa Kabila la Wagongwe.2.⁠ ⁠Lukas Moses Msaga - Mtoto wa Mtemi Sigulu anayefundishwa kurithi mikoba ya Mtemi Sigulu.⁠3.⁠ ⁠⁠Askari Uhifadhi Daraja la Pili - Kimori Shiwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ikolojia, Hifadhi ya Taifa Katavi. Endelea kutufuatilia kupitia Platifomu za TANAPA Podcast.TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.
    --------  
    54:47
  • TANAPA PODCAST EPISODE 12 - Zoezi la Uhamishaji Tembo kutoka Misenyi kwenda Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato.
    Episodi hii imeangazia zoezi endelevu la kuwahamisha tembo walowezi kutoka maeneo ya karibu na wananchi kwenda hifadhini na zoezi zima la kuwaswaga tembo waliotoka hifadhini kuvamia maeneo ya wananchi na kuwarudisha hifadhini.Sikiliza Episodi hii kwa taarifa hiyo na mengine mengi kupitia Epsode ya 12.Eneo: Misenyi - Bukoba.Host: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine MbenaGuests: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Dkt. Fredrick Mofulu - Mkuu wa Hifadhi Ibanda - Kyerwa. NaKamishna Msaidizi wa Uhifadhi Charles Ngendo - Mkuu wa Hifadhi Rumanyika - Karagwe.Fuatilia kupitia Platform za TANAPA Podcast.
    --------  
    50:02

More Government podcasts

About TANAPA PODCAST

Karibu katika Podcast rasmi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), inayoangazia mazungumzo ya kina kuhusu Uhifadhi wa Maliasili zilizopo ndani ya Hifadhi za Taifa, Elimu ya Uhifadhi, Utalii pamoja na Fursa za Uwekezaji. Vipindi vya Podcast hii vinajadili mikakati ya uhifadhi endelevu, ukuaji wa utalii, na ushirikiano na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuhakikisha Rasilimali za Taifa zinatunzwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Podcast website

Listen to TANAPA PODCAST, Inside Briefing with the Institute for Government and many other podcasts from around the world with the radio.net app

Get the free radio.net app

  • Stations and podcasts to bookmark
  • Stream via Wi-Fi or Bluetooth
  • Supports Carplay & Android Auto
  • Many other app features
Social
v8.0.7 | © 2007-2025 radio.de GmbH
Generated: 12/7/2025 - 5:59:41 PM